MISS TOURISM TANZANIA INTERNATIONAL

MISS TOURISM TANZANIA INTERNATIONAL
Miss Tourism Tanzania Pageants

Miss Tourism Tanzania Pageant

Miss Tourism Tanzania Pageant
We Welcome Miss Tourism Tanzania Organisation

Miss Tourism World 2005- Africa

MISS TOURISM TANZANIA PAGEANT

Serikali imeimwagia pongezi Miss Utalii Tanzania 2013.




Baada ya kukwama kwa Muda Mrefu Kutokana na baadhi ya wadhamini kushindwa kutimiza ahadi zao za udhamini hatimaye Bodi ya Mashindano ya Miss Utalii Tanzania imepata kibali cha fainali za Miss Utalii Tanzania 2012/13 kufanyika 11-5-2013 na za awali kufanyika 4-5-2013. 

Taratibu zote za fainali za Taifa kufanyika Tarehe hiyo zimekamilika kwa mujibu wa sheria na za nchi,taratibu na kanuni ya mashindano haya.Waandaaji wamewasilisha na kukabidhi serikalini uthibitisho wa wadhamini wa zawadi kwa washindi, sambamba na mikataba ya kulinda haki za washindi na waandaaji ,ikiwemo haki za kupewa zawadi bila ya kukosa.

Baada ya kibali kutolewa na serikali, sasa washiriki wote wa fainali hizi , watafanya ziara za kutangaza utalii ,utmaduni,na mianya ya uwekezaji katika mikoa ya Tanga,Pwani,Lindi na Dar es salaam kuanzia jumatatu ya 30-5-2013. Ziara hii itatoa fulsa ya pekee kwa mikoa hiyo kujitangaza kitaifa na kimatifa kupitia mashindano haya.

 Wakati huo serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imewapongeza juhudi zinazo fanywana Waandaaji wa Miss Utalii Tanzania  za kutangaza vivutio vya utalii na utamaduni wa Tanzania kitaifa na kimataifa kwa kuipatia Sifa kubwa Tanzania kupitia mashindano hayo. Kwa mujibu wa maelezo ya Barua ya Tarehe 19.04.2013 iliyo sainiwa na Ndugu Z. A Kimwaga kwa niaba ya Katibu mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii kwenda kwa waandaaji wa Miss Utalii Tanzania. Wizara na serikali kwa ujumla inatambua juhudi zinazofanywa na waandaaji wa mashindano haya katika kukuza utalii wa ndani na Utalii wa Kitamaduni.

Katika kuthibitisha hilo Wizara imewashauri waandaaji wa mashindano hayo kuwaslisha maoombi ya msaada kutoka serikalini kwa wakati na kwa kuzingatia misimu na Bajeti ta serikali ili kuwe na uwezekano wa serikali Kudhamini mashindano hayo. Hata hivyo Serikali kupitia Taasisi zake za Mamlaka ya Hifadhi ya Taifa(TANAPA) , Mamlaka ya Ngorongoro(NCIA), na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) kwa miaka yote ikiwepo mwaka huu imekuwa ikitoa udhamini wa Hali na Mali katika kufanikisha Mashindano hayo.
Nae Rais wa Mashindano hayo Gidion Chipungahelo kwa niaba ya Bodi ya Mashindano amewaomba Radhi watanzania wote , wadau w ashindano , washiriki, wadhamini na wengine wote walioguswa au kuathiriwa kwa namna yoyote.

2 comments:

Anonymous said...

Let's think of words that sound dirty but really aren't.
If you don’t have much skill in programming, but still think that creating and developing games
is the most suitable for you, there are special
courses that will give you training in graphic designing, game development, and computer
animation. As ever we strive to help our customers make informed decisions and understand where their r4 cards are coming from.



Stop by my homepage ... http://adpower.x-y.net/xe/545719

Anonymous said...

Your video from Viddler is downloaded to your local disk.
If you would rather keep the process simple,
or have a need to save streaming FLVs to your Android phone that aren't available on You - Tube, your best option is the useful web-based service Keep - Vid. In the resulting window you will be able to use either the Save to button beneath the video clip or the ghosted download icon in the lower left corner of your display (a down-pointing arrow).

Also visit my weblog ... http://clinichu.com/